KISWAHILI F1 ANNUAL 2020

 Ku-Download mtihani huu [ BOFYA HAPA ]

JAMHURI YA MUUNGANO YA TANZANIA

OFISI YA RAIS

SERIKALI ZA MITAA NA TAWALA ZA MIKOA

MTIHANI WA MUHULA WA MWISHO

KIDATO CHA KWANZA

KISWAHILI

                  

MUDA: Saa 2 ½                                                                                                          DEC, 2020.

Maelekezo:

-          Mtihani huu una sehemu A, B, C na D

-          Jibu maswali yote kwenye karatasi ya maswali

-          Zingatia maelekezo ya kila sehemu na kila swali

-          Dumisha usafi na uepuka kufutafuta ovyo ili usipunguziwe alama utakazopata

 

 

SEHEMU A – UFAHAMU (alama 20)

 

1.      Soma kifungu cha habari kifuatacho kisha ujibu maswali yatakayofuata

 

Kwa hakika usilolijua ni sawa na usiku wa giza...............wengi hawakuamini kuwa walichokisikia ndicho kilichokuwa kikitokea, hasa kwa wale waliokosa fursa ya kuliona tukio hilo la kusikitisha kwa macho yao, hao ni wale waliosikia sauti ya mirindimo iliyorindima mithili ya ngurumo za mvua.  Iliwawia vigumu pia kukubali kuwa sauti hizo zilizoshitua nyoyo na kujenga taharuki miongoni mwa watu, ziliandamana na miale mekundu ya moto!  Ndiyo maana watu hao waliendelea na shughuli zao kama kawaida, punde matendo yao yalisimamishwa na mrindimo mkubwa uliozua kishindo na kuthubutu kutingisha kuta, madirisha na hata kutiririsha mchanga na vumbi jembamba kutoka kwenye mapaa ya nyumba zilizokuwa masafa fulani kutoka kitongoji kilichokumbwa na mkasa huo.

 

Baada ya dakika chache walionekana raia wa vijiji  vya jirani wakiwa kwenye hali ya mfadhaiko, bila ya shaka walikuwa wakitafuta kimbilio la haraka ili kusalimisha maisha yao.  Ilikuwa kama mchezo wa kuigiza.....................huyu anapenya hapa .............yule anatokomea kule..............hawa wameshikana mikono, lakini wamepoteza matumaini...........ilimradi mambo yalikuwa hayaelezeki kwa lugha ya kawaida.

Ingawa mtafaruku huo ulitawala kwenye nafsi ya kila aliyekuwa hapo, lakini hali ya mandhari ya usiku huo ilikuwa na mvuto wa kupigiwa mfano.....ukitupa macho mbinguni ulikuwa unatazamana na mawingu meupe yaliyokuwa yakijikokota kwa mbwembwe pembezoni, nyota nazo zilionesha ushirikiano

 

kwa kujimwaga moja moja na kumetameta kwa zamu, mwezi nao haukuwa

nyuma kwani uliamua kufungulia nuru yake iliyokuwa ikiadhimisha maulidi matakufu ya Mtume (rehema ziwe juu yake).  Hali hii ilikuwa ni faraja kwa wale waliotokomea vichakani au kwenye viunga vya mji vilivyotelekezwa na mgao wa umeme ambao huzaa giza nene lisilovumilika.

 

Kwa kuwa sakata hili liliwakumbusha wananchi wengi kurejea kwa muumba wao angalau kwa saa chache, kwa sala na maombi yaliyowasilishwa kwake kwa dhati na masikitiko ingawa yalikuwa kwenye maneno yaliyosema kwa lugha tofauti tofauti za kikabila lakini yalifika kwa maulana naye akaridhia kwa kutoa majibu yaliyorudisha amani na utulivu iliyokuwa imepotea kwa wastani wa saa tano hivi.

 

Kwa kila msamaria mwema hana budi kuwapa pole wakaazi wote wa Gongo la Mboto na vitongoji vya jirani pamoja na kuwaunga mkono kwa hali na mali ili nao waamini kuwa baada ya dhiki faraja, kutokana  na tukio la 05/08/2019

 

 

Maswali

i)       Pendekeza kichwa cha habari kisichozidi maneno matano kisha ukiandike kwa herufi kubwa na upigie mstari .......................................................................................................................................

 

ii)     Taja methali iliyojitokeza kwenye aya ya mwisho ..............................................................................

 

iii)  Taja maana ya maneno yafuatayo kama yalivyotumika kwenye kifungu

a)         Mbwembwe ..................................................................................................

b)        Kumetameta .................................................................................................

c)         Sakata ...........................................................................................................

d)        Ngurumo ......................................................................................................

e)         Maulana .......................................................................................................

 

iv)   Tarehe 05/08/2019 kulitokea nini kwenye maeneo yaliyotajwa katika habari uliyosoma?

......................................................................................................................................................................................................................................................................................................................

 

v)      Kihistoria tukio lililoelezwa kwenye kifungu linakukumbusha kitu gani kilichowahi kutokea jijini Dar es Salaam

......................................................................................................................................................................................................................................................................................................................

 

vi)   Chagua jibu sahihi kati ya haya “watu waliodhurika kutokana na tukio lililoelezwa kwenye kifungu wanaitwa”

a)      Wahanga

b)      Waathirika

c)      Watuhumiwa

d)      Wazembe

vii) Taja madhara matano ambayo huwapata watu wanaofikwa na mkasa ulioelezwa kwenye kifungu

a)        ..................................................................................................................................................................................................................................................................................

b)        ..................................................................................................................................................................................................................................................................................

c)        ..................................................................................................................................................................................................................................................................................

d)        ..................................................................................................................................................................................................................................................................................

e)        ..................................................................................................................................................................................................................................................................................

 Ku-Download mtihani huu [ BOFYA HAPA ]

SEHEMU B (alama 25)

UTUMISHI WA LUGHA NA USAHIHI WA WAANDISHI

 

2.    a)  Sentensi zifuatazo zimeandikwa kwa kukiuka kanuni za lugha.  Ziandike upya ili kurekebisha makosa

i)         Mama inafanya kazi ofisini ....................................................................

ii)       Kasimu kazuri kamepotea ............................................................................................................

iii)     Mdada mmoja amepatwa na ajali ...............................................................................................

iv)     Juma haujambo? ..........................................................................................................................

v)        Jana tulicheza mpira kwa muda wa lisaa limoja. .........................................................................

 

b)   i)  Lugha ni ...................................................................................................................

....................................................................................................................................................................................................................................................................................................  

 ii) Kielezi huelezea kuhusu

a)        ...........................................................................................................................

b)        ...........................................................................................................................

c)        ...........................................................................................................................

 

 iii) Taja mambo mawili ambayo unaamini yangetokea iwapo tusingekuwa na lugha kwenye jamii

a)        ............................................................................................................................................................................................................................................................................

b)        ............................................................................................................................................................................................................................................................................

 

SEHEMU C (alama 25)

SARUFI

 

3.    a)    Ainisha maneno kwenye sentensi zifuatazo kwa kuweka alama ya neno husika chini yake

i)         Uzima wa mtu ni afya

.................................................................................................................

ii)       Penye mafanikio ndipo niendapo

..................................................................................................................

iii)     Watoto wangu hawa wawili warefu sana wamefaulu

................................................................................................................

iv)     Unanukia ingawa hauna ladha nzuri

..................................................................................................................

v)        Msaada wako umenifaa. Asante!

.................................................................................................................

 Ku-Download mtihani huu [ BOFYA HAPA ]

b)    Sarufi ina dhima nyingi.  Taja mbili kati ya hizo

a)      ....................................................................................................................................................................................................................................................................................

b)      ....................................................................................................................................................................................................................................................................................

 

c)   Taja aina nne (4) za vielezi

i)       ........................................................................................

ii)     ........................................................................................

iii)   ........................................................................................

iv)   ........................................................................................

 

 

SEHEMU D

FASIHI (alama 30)

  1.  a)   Tegua vitendawili vifuatazo

i)           Hausimiki  hausimami ........................................................................................................

ii)         Mzungu anamlamba Mwafrika ..........................................................................................

iii)       Pita huku nipite huku tukutane kwa mjomba ....................................................................

iv)       Wanangu wawili wanafukuzana lakini hawakutani ...........................................................

v)          Vibibi viwili viko mlimani vyapeta.......................................................................................

 

b)    Kauli zifuatazo zinamaana gani?

                  Mfano:  Juma ameasi ukapera

                   Maana:  Juma ameoa

i)           Chogo “ana mkono wa birika”

Maana: .................................................................................................

ii)         Masanja “amefulia”

Maana: .................................................................................................

iii)       Bwege hana “noma”

Maana: .................................................................................................

iv)       Mshahara wenyewe “mkia wa mbuzi”

Maana: .................................................................................................

v)          Huyu ndiye “mkali wao”

Maana: .................................................................................................

 

c)    Kamilisha metheali zifuatazo

i)           Subira ............................................heri

ii)         Penye nia .......................................................................................

iii)       .........................................pema ....................................panamwita

iv)       Chema ............................................kibaya ....................................

v)      Baniani ........................... ..........................chake ...........................